2 Corinthians 4:1-6

Hazina Ya Mbinguni Katika Vyombo Vya Udongo

1 aKwa hiyo, kwa kuwa tuna huduma hii kwa rehema za Mungu, hatukati tamaa. 2 bTumekataa mambo ya siri na ya aibu, wala hatufuati njia za udanganyifu, tukichanganya Neno la Mungu na uongo. Kinyume cha hayo, tunadhihirisha kweli waziwazi na kujitambulisha wenyewe kwenye dhamiri ya kila mtu mbele za Mungu. 3 cHata nayo Injili yetu kama imetiwa utaji, ni kwa wale tu wanaopotea. 4 dKwa habari yao, mungu wa dunia hii amepofusha akili za wasioamini, ili wasione nuru ya Injili ya utukufu wa Al-Masihi, aliye sura ya Mungu. 5 eKwa maana hatujihubiri sisi wenyewe ila tunamhubiri Isa Al-Masihi kuwa ni Bwana na sisi ni watumishi wenu kwa ajili ya Isa. 6 fKwa kuwa Mungu, yeye aliyesema, “Nuru na ing’ae gizani,” ameifanya nuru yake ing’ae mioyoni mwetu ili kutupatia nuru ya maarifa ya utukufu wa Mungu katika uso wa Al-Masihi.

Copyright information for SwhKC